Tuesday, September 5, 2017

Availabilities and accessibilities of health facilities compared to population between Dar es Salaam and the whole Country (Tanzania).


Dar es Salaam is unquestionably the epicenter and the hub of human activities in Tanzania. Its strategic location in business, employment and recreation has attracted residence of over 10% of Tanzanian population. Even though it is not the country’s capital currently almost all the diplomatic offices, governmental and Nongovernmental institutions are headquartered in Dar es Salaam hence creating a meandering ground for both national and international migrants.
Ideally the population size should concurrently grow along with infrastructures, this includes health facilities. Sadly this is not the reality for Dar es Salaam. The health facilities in Dar es Salaam are extremely overloaded than the general average for distribution in Tanzania based on population. Accordance to huru Map statistics based on 2014 research, one dispensary in Dar es Salaam is burdened with 12,952 people while the country’s average distribution is one dispensary to 7,596 people. One health center in Dar es Salaam serves 112,365 people as one health center in Tanzania serve 62,662 people.
There are approximately seven hospitals in Dar es salaam, with the population in Dar, if all residents depend on these seven hospitals then one hospital will serve 593,928 people while one hospital in Tanzania serves 170,832 people, therefore demand for health services in Dar is huge than the rest of the country. Moreover one clinic serves 1,039,375 people in Dar es Salaam while one clinic serves 255,278 people in Tanzania.

There is challenge when it comes to distribution of Health workers across the country; with over 4 million people residing in this city, one medical officer in Dar es salaam attends to 42,423 people while the same officer in Tanzania attend to an average of 26,290 people, a clinical assistant in Dar es Salaam attends to 83,150 people while the same clinical assistant should attend to 36,948 people in rest of the country. One assistant medical officer in Dar es Salaam attends to 57,743 people while the same assistant should attend to 25,866 people in Tanzania, one nutrition officer who works in Dar es Salaam should attend to 1,385,833 people and the same officer should attend to 748,815 people in the whole country.
Another factor stressing the need of allocating more health centers in Dar es Salaam especially clinic and hospitals with health specialists is the ratio of traffic and crime incidents, 8 deaths occur in every 100,000 population in Dar es salaam which is exact the same figures in Tanzania. Number of road accidents is about two-fifths to the figure of Tanzania; number of deaths caused by road accidents in Dar es Salaam is about 10% of same kind of deaths in Tanzania.
The above facts press an urgent alarm to the government and health stakeholders to respond to this matter without delay. Health security is a vital element towards development of any kind. By considering the contribution of Dar es Salaam to the national income, improvement of health facilities in the city becomes crucial.

Friday, April 7, 2017

Utoaji mimba( abortion)





 







Mimba kutoka ni tokeo la mambo tofautitofauti, kama matumizi ya kemikali au kwa mjamzito  ambazo zina kemikali zinazosababisha mimba kutoka endapo zitatumiwa bila maelezo sahihi kutoka kwa mtaalamu wa afya, Dawa nyingi zinazotibu magonjwa mbalimbali zinaonyesha wazi kwamba mwanamke mjamzito anaruhusiwa ama la, na hata akiruhusiwa zinaeleza kwamba atumie chini ya uangalizi wa mtaalamu wa afya.
Lakini Kutoa mimba kwa kusudia endapo mwanamke hana utayari wa kulea mimba au hajajiandaa kupata mtoto kwa wakati huo ni Moja ya vitu ambavyo Wanawake wengi wanajihusisha navyo, napengine kuhofia namna ambavyo jamii itawatazama hufanya mambo haya kwa kujificha sana hii huwafanya wengi kutoa mimba kiholela na kuhatarisha maisha yao.

Hatua za utoaji Mimba
Mimba changa ambayo tayari ipo kwenye mji wa mimba hutolewa kwa kutumia kemikali zilizo kwenye madawa,au vifaa maalum vinapitishwa njia ya uzazi wa mwanamke mpaka kwenye mfuko wa uzazi na kuanza kutoa kitoto ndani ya mji wa uzazi.

Njia salama  ya utoaji mimba huwahusisha wataalamu wa afya ya uzazi na njia za kiholela mtoaji mimba hutumia njia zisizo rasmi na kuharibu mimba.

Uhalali wa Utoaji Mimba
Sheria za dini kama dini ya kikristo hairuhusu utoaji mimba.
Kuna baadhi ya sheria za nchi Kama Tanzania ambazo haziruhusu kabisa utoaji wa mimba lakini katika nchi zilizo endelea kama marekani sheria zinaruhusu utoaji mimba salama.

Madhara ya utoaji mimba 
Ni kama vifo,ugumba na utasa kwa mwanamke,pia mwanamke anaweza kuathirika kisaikolojia kutokana na mawazo ya kuharibu nakuuwa kiumbe kisichokuwa na hatia.

Epuka ngono zembe, tumia njia za uzazi wa mpango, epuka kufanya mapenzi kabla ya ndoa kuepuka utoaji haramu wa mimba.
Tafuta washauri wa afya pale utakapo gundua kuwa na mimba ili upate ushauri thabiti wa nini cha kufanya.

 Picha zifuatazo zinaonyesha viumbe au mimba changa zilizokatishwa maisha na haki ya kuishi.







MAONI YA MWANDISHI 
Wakati wewe unatoa mimba kuna watu wanahangaika kutafuta watoto, wanavunja mahusiano ama ndoa kwa kukosa watoto, wanakesha wakiomba kutafuta watoto, kama umepata ujauzito bila kupanga ni bora ukazaa na ukatafuta watu wenye uhitaji na kuwa adopt watoto kuliko kuua.

Hakuna haja yakupata ujauzito kama huwezi kuikuza mimba tumia njia za uzazi wa mpango ili ujiepushe kuua kiumbe kisicho na hatia kwa starehe zako binafsi.


MAGONJWA YA NGONO

 Muandishi, Dr. Gaudence Mathew


Magonjwa ya ngono ni kundi la magonjwa ambayo huenezwa kwa njia ya kujamiana/kukutana kimwili/kufanya tendo la ndoa.
Kuna aina nyingi za magonjwa ya ngono na yamegawanyika katika makundi kulingana na dalili na alama yanazosababisha
MAGONJWA YANAYOSABABISHA KUTOKWA NA UCHAFU/USAHA SEHEMU ZA SIRI

– KISONONO (GONORRHEA)
– KLAMADIA (CHYLAMADIA)JAMII YA KISONONO
– FANGASI (GENITAL CANDIDIASIS)
– TRAKOMONIASISI (TRACOMONIASIS)
– KISAMAKI 

 DALILI ZAMAGONJWA YANAYOSABABISHA KUTOKWA UCHAFU/USAHA SEHEMU ZA SIRI

• Kutokwa uchafu/usaha sehemu za siri.
• Maumivu makali ya tumbo lote(wanawake).
• Kuwashwa sehemu za siri
• Maumivu chini ya kitovu (wanawake)
• Maumivu wakati wa kujamiana
• Maumivu makali wakati wa kukojoa(hasa wanaume)

MADHARA YA MAGONJWA YANAYOSABABISHA KUTOKWA UCHAFU/USAHA SEHEMU ZA SIRI
Kwa wanawake:-

Uke Ulioathirika

• Uambukizo kwenye pango la nyonga(PID)
• Ugumba/utasa.(INFERTILITY)
• Mimba kutunga nje ya tumbo la uzazi.(ECTOPIC PREGNANCY)
• Maumivu makali ya tumbo(PERITONITIS)
Kwa wanaume.
• Kuziba mkojo,(URETHRAL STRICTRES)
• Kuvimba mapumbu(ORCHITIS)
• Utasa. (INFERTILITY)

Kwa watoto wachanga:-Kutokwa usaha kwenye macho na Upofu

Mtoto alie athirika na Ugonjwa wa Ngono akiwa Tumboni




Monday, July 16, 2012

Mlo kamili(Balance diet)


-->

mlokamili wenye virutubisho vyote ukizingatiwa unasaidia kuepukana na magonjwa kama saratani, kisukari, magonjwa ya moyo na magonjwa ya mifupa.
Zingatia yafuatayo.

PATA KIFUNGUA KINYWA KIZURI

Wahenga wanashauri kwamba pata kifungua kinywa chenye hadhi ya kifalme,chakula cha mchana (lunch) kama mtoto wa mfalme na chakula cha usiku (dinner) kama mtumwa, ukipata kifungua kinywa cha nguvu asubuhi itakusaidia kufanya kazi zako wa umakini zaidi na pia itasaidia kubudget pesa yako kwani hutakuwa na ulazima wakununua vitu vidogodogo vya kula.

Pata milo mitatu kwa siku kila siku

Nimuhimu kuzingatia hili kwani kwakufanya hivi utakuwa ni mwenye nguvu sikunzima,hivyo kuepuka matatizo ya tumbo hasa vidonda vya tumbo.



Pika chakula wewe mwenyewe kuliko kununua

Nunua viungo mbalimbali vitavyokusaidia wakati wakujitayarishia chakula,kujipikia kunapunguza gharama na pia ni nafuu, pia itakusaidia kupika chakula katika kiwango unachotaka,kama vile kiasi cha chumvi, kwani ni nzuri zaidi chumvi ikiivia jikoni kuliko ikiongezewa wakati wa chakula, vilevile inasaidia kufanya mabo yako kwa usafi zaidi kwakuwa mtu yeyote mwenye akili timamu atajali afya yake.

Chakula cha usiku.

Nivizuri kupata chakula chepesi ili kusaidia mmengenyo wa chakula usiku ukiwa umelala kasi ya mmeng'enyo hupungua tunapokuwa tumelala.

Kula matunda kwa wingi

 


Nivizuri kula matunda kwa wingi itakusaidia kuongeza vitamins, na kuukinga mwili na magonjwa.

Kunya maji mengiItakusaidia katika mmeng'enyo wa chakula,kusafisha tumbo pamoja nakusaidia utoaji taka mwilini







Thursday, July 12, 2012

Matumizi ya asali katika tasnia ya urembo (the use of honey in the beauty industry)
                Asali inatibu chunusi (honey treats acne)


Mazao asilia ya mimea na matunda vilevile mazao yanayotoka kwa wanyama ni njia salama zaidi ya kutibu chunusi.lakini pia asali ni njia nzuri ya kutibu chunusi, kuondoa mabaka na kufa

nya ngozi yako iwe laini.


Mchanganyiko wa asali na mdalasini yanaweza kutumika kutibu chunusi

Hapa ni jinsi ya kutumia asali na mdalasini kutibu chunusi: Chunusi ni tatizo linalowasumbua watu wa umri mbalimbali, vijana kwa watu wazima na jinsia zote, matumizi

Asali kijiko kimoja, unga wa mdalasini kijiko kimoja, changanya vizuri kisha upake eneo lililo athirika safisha uso na maji ya uvuguvugu baada ya dakika ishirini.




Tafadhali kumbuka
fanya  hivyo mwenyewe. Kama utasikia ngozi kuwasha tafadhali acha kutumia.Dawa hii inaweza kufanya kazi kwa kila mtu. Tiba hii hufanya kazi  kwa aina mbalimbali ya ngozi.


Unaweza pia ukalala na kipako ulichopaka yaani mchanganyiko uliouandaa baada yakukauka kisha asubuhi ukaosha uso kwa maji ya uvuguvugu.