Friday, April 7, 2017

MAGONJWA YA NGONO

 Muandishi, Dr. Gaudence Mathew


Magonjwa ya ngono ni kundi la magonjwa ambayo huenezwa kwa njia ya kujamiana/kukutana kimwili/kufanya tendo la ndoa.
Kuna aina nyingi za magonjwa ya ngono na yamegawanyika katika makundi kulingana na dalili na alama yanazosababisha
MAGONJWA YANAYOSABABISHA KUTOKWA NA UCHAFU/USAHA SEHEMU ZA SIRI

– KISONONO (GONORRHEA)
– KLAMADIA (CHYLAMADIA)JAMII YA KISONONO
– FANGASI (GENITAL CANDIDIASIS)
– TRAKOMONIASISI (TRACOMONIASIS)
– KISAMAKI 

 DALILI ZAMAGONJWA YANAYOSABABISHA KUTOKWA UCHAFU/USAHA SEHEMU ZA SIRI

• Kutokwa uchafu/usaha sehemu za siri.
• Maumivu makali ya tumbo lote(wanawake).
• Kuwashwa sehemu za siri
• Maumivu chini ya kitovu (wanawake)
• Maumivu wakati wa kujamiana
• Maumivu makali wakati wa kukojoa(hasa wanaume)

MADHARA YA MAGONJWA YANAYOSABABISHA KUTOKWA UCHAFU/USAHA SEHEMU ZA SIRI
Kwa wanawake:-

Uke Ulioathirika

• Uambukizo kwenye pango la nyonga(PID)
• Ugumba/utasa.(INFERTILITY)
• Mimba kutunga nje ya tumbo la uzazi.(ECTOPIC PREGNANCY)
• Maumivu makali ya tumbo(PERITONITIS)
Kwa wanaume.
• Kuziba mkojo,(URETHRAL STRICTRES)
• Kuvimba mapumbu(ORCHITIS)
• Utasa. (INFERTILITY)

Kwa watoto wachanga:-Kutokwa usaha kwenye macho na Upofu

Mtoto alie athirika na Ugonjwa wa Ngono akiwa Tumboni




1 comment:

  1. How to win real money in casinos | JDKH
    To take a closer look at some of the best and most trusted online 동해 출장샵 casinos in the 김제 출장샵 world, 김제 출장샵 고양 출장마사지 With online slots, live casino games, 제주 출장마사지 and much more,

    ReplyDelete